Ikiwa inaongoza katika msimamo wa ligi kuu nchini klabu ya Yanga sc imeendelea na maandalizi kuelekea mchezo dhidi ya klabu ya Kmc utakaofanyika machi 19 katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.
Kocha wa klabu hiyo mwenye uraia wa Tunisia Nasreddine Nabi tayari anafurahia urejeo wa mastaa wake Saido Ntibanzokiza,Khalid Aucho na Farid Musa huku winga Chico Ushindi akiwa njiani kupona marelia yanayomsumbua na kumfanya akose mchezo uliopita dhidi ya Geita Gold Fc uliofanyika katika uwanja wa Ccm Kirumba ambapo Yanga sc waliibuka na ushindi wa 1-0.
Kuhusu mchezo kocha Nabi alisema“Kila mtu anajua uwezo wa KMC, hii ni miongoni mwa timu bora kwenye ligi kuu na ni wazi tunatarajia mchezo mgumu dhidi yao, hasa kutokana na ukweli kuwa sehemu kubwa ya kikosi chao kina wachezaji wazoefu.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
“Lakini licha ya ushindani tunaotarajia kukumbana nao ni lazima tuhakikishe tunashinda mchezo huu, nilazima mawazo yetu yawe juu ya pointi tatu na si matokeo ya aina nyingine na wachezaji wangu wanajua hilo.”Alimalizia kocha huyo anayesifika kwa kupenda nidhamu ya hali ya juu.