Home Makala Yanga Sc Kuachana na Musonda

Yanga Sc Kuachana na Musonda

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imefikia makubaliano ya kuachana na mshambuliaji Kennedy Musonda ambaye mkataba wake unaelekea ukingoni msimu huu.

Staa huyo aliyesajiliwa miaka mitatu  iliyopita kutokea klabu ya Power Dynamos ya nchini kwao Zambia ambapo ilitarajiwa angekua mbadala wa mshambuliaji Fiston Mayele aliyeondoka klabuni hapo msimu mmoja uliopita na kujiunga na Pyramid Fc.

banner

Hata hivyo Musonda ameshindwa kuwa na uhakika wa nafasi pamoja na Mayele kuondoka klabuni hapo ambapo amekua akianza mara chache na muda mwingine akikosa nafasi kabisa.

Mabosi wa Yanga sc pamoja na kumleta Prince Dube msimu huu pia wanaona ni vyema kuongeza nguvu eneo la ushambuliaji ambapo wanamtolea macho Jonathan Sowah wa Singida Black Stars.

Tayari mshambuliaji huyo ameshapewa taarifa kuhusu kutoongezewa mkataba na mabosi wa klabu hiyo na ndio sababu ya kufuta picha nyingi akiwa na klabu hiyo katika mtandao wake wa Instagram.

Sasa Musonda anaangalia ofa alizonazo ili aamue atajiunga na klabu gani msimu ujao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited