Home Makala Yanga sc Yabanwa Kigoma

Yanga sc Yabanwa Kigoma

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imeshindwa kuibuka na ushindi katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ruvu Shooting uliofanyika katika uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma baada ya mchezo huo kumalizika kwa suluhu.

Yanga sc haina budi kumshukuru mshika kibendera ambaye alikataa goli la Ruvu Shooting akidai kuwa mfungaji alikua ameotea na kuwafanya Yanga sc waendelee kubaki mchezoni mwanzoni mwa kipindi cha kwanza.

Mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika mchezo ulikua suluhu huku Ruvu Shooting wakishukuru baada ya Fiston Mayele kugongesha mwamba mara mbili akijaribu kumfunga golikipa Mohamed Makaka.

banner

Kutokana na msimamo huo Yanga sc anafikisha alama 56 huku akifuatiwa na Simba sc yenye alama 43 ikiwa na mchezo mmoja mkononi huku Ruvu Shooting ikiwa katika nafasi ya 13 ya msimamo wa ligi kuu nchini ikiwa na alama 22.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited