Home Makala Yanga sc Yafungukia Ujio wa Migne

Yanga sc Yafungukia Ujio wa Migne

by Sports Leo
0 comments

Mkurugenzi wa Uwekezaji GSM Injinia Hersi Said ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindao Yanga, amesema wanaendelea na mchakato wa kusaka kocha mpya atakayerithi mikoba iliyoachwa na Cedric Kaze

Kumekuwa na tetesi kumuhusu kocha wa zamani wa Harambee Stars na Guinea ya Ikweta Sebastian Migne anayetajwa kumalizana na mabingwa hao wa kihistoria

Hersi amesema Migne ni miongoni mwa makocha wanaofanya nao mazungumzo lakini bado hawajafikia mwafaka

banner

“Ni kweli, Migne ni miongoni mwa makocha ambao tuko katika mazungumzo nao, lakini hayuko peke yake, wengine wapo pia. Bado mwafaka haujafikiwa kuamua yupi tumkabidhi timu, “alisema Hersi

Awali Yanga ilikuwa na mpango wa kumuachia timu kocha Juma Mwambusi mpaka mwishoni mwa msimu

Hata hivyo wamebadili ‘gia angani’ wakiamua kumleta kocha mpya ambaye atafanya kazi na Mwambusi ili hata pale ligi itakapomalizika atakuwa amefahamu uimara na madhaifu ya timu yako wapi ili imsaidie katika kufanya maboresho

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited