Klabu ya Yanga sc sasa itatumia uwanja wa Chamazi Complex kama uwanja wa nyumbani katika mchezo wa kombe la shirikisho la AzamTv baada ya uwanja wa Benjamin Mkapa kuwa katika matengenezo kwa muda.
Yanga sc itautumia uwanja huo unaomilikiwa na klabu ya Azam Fc katika mchezo wa siku ya ijumaa dhidi ya Tanzania Prisons mchezo wa hatua ya mtoano ya kombe la shirikisho unaotarajiwa kuanza majira ya saa moja usiku.
Pamoja na hayo bado klabu ya Yanga sc itaendelea kuutumia uwanja wa Benjamini Mkapa kama uwanja wa nyumbani katika michuano ya kimataifa dhidi ya Real Bamako utakaofanyika siku ya Jumatano march 8.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.