Kwa mara ya pili klabu ya Yanga sc imefanikiwa kupata ushindi mnono baada ya ule dhidi ya Zalan Fc ambapo wameifunga timu ya Rhino Rangers ya mkoani Tabora kwa mabao 7-0 huku Kennedy Musonda akifanikiwa kufunga kwa mara ya kwanza tangu asajiliwe.
Mvua ya magoli ilianzishwa na Dickson Ambundo dakika ya 7 kisha Kennedy Musonda alifunga mabao dakika za 16 na 46 huku Farid Mussa alifunga dakika ya 25 baada ya Aziz Ki kufunga dakika ya 20 huku Yannick Bangala nae akifunga dakika ya 26 na bao la mwisho la Yanga sc lilifungwa na David Bryson dakika ya 90+3.
Yanga sc baada ya ushindi huo sasa imefanikiwa kufuzu hatua inayofuatia ikiungana na timu nyingi za ligi kuu kufuzu huku ikitarajiwa kukutana na Tanzania Prisons katika hatua hiyo inayofuatia.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.