Home Makala Yanga sc Yaipiga 7-0 Rhino Rangers

Yanga sc Yaipiga 7-0 Rhino Rangers

by Sports Leo
0 comments

Kwa mara ya pili klabu ya Yanga sc imefanikiwa kupata ushindi mnono baada ya ule dhidi ya Zalan Fc ambapo wameifunga timu ya Rhino Rangers ya mkoani Tabora kwa mabao 7-0 huku Kennedy Musonda akifanikiwa kufunga kwa mara ya kwanza tangu asajiliwe.

Mvua ya magoli ilianzishwa na Dickson Ambundo dakika ya 7 kisha Kennedy Musonda alifunga mabao dakika za 16 na 46 huku Farid Mussa alifunga dakika ya 25 baada ya Aziz Ki kufunga dakika ya 20 huku Yannick Bangala nae akifunga dakika ya 26 na bao la mwisho la Yanga sc lilifungwa na David Bryson dakika ya 90+3.

Yanga sc baada ya ushindi huo sasa imefanikiwa kufuzu hatua inayofuatia ikiungana na timu nyingi za ligi kuu kufuzu huku ikitarajiwa kukutana na Tanzania Prisons katika hatua hiyo inayofuatia.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited