Home Makala Yanga Sc Yamtambulisha Chikola

Yanga Sc Yamtambulisha Chikola

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Yanga sc imemtambulisha rasmi mchezaji Offen Chikola ambaye amejiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili akiwa kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Tabora United.

Chikola amesaini klabuni hapo baada ya kuonyesha kiwango bora msimu ulioisha wa ligi kuu akifunga mabao saba pamoja na kuwa ni kiungo wa pembeni nafasi aliyocheza msimu mzima.

banner

Mabosi wa Yanga sc wamekamilisha usajili huo ikitajwa kuwa anakwenda kuchukua nafasi ya Farid Mussa ama Dennis Nkane ambao wanaweza kuondolewa klabuni hapo kutokana na kukosa nafasi ya kucheza mara kwa mara.

Chikola anatarajiwa kuiongezea kasi safu ya ushambuliaji ya klabu hiyo akiungana na Clement Mzize na Prince Dube katika safu ya ushambuliaji ya klabu hiyo huku wakisaidiwa na Pacome Zouzoua atakayekua anacheza kama namba kumi akichukua nafasi ya Stephan Aziz Ki aliyeuzwa.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited