Home Makala Yanga sc Yamtambulisha Gift

Yanga sc Yamtambulisha Gift

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Yanga sc imemtambulisha beki Gift Fred ambaye imemsajili kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya S.C Villa ya nchini Uganda inayoshiriki ligi kuu nchini humo.

Yanga sc imemsajili beki huyo wa katikati ambaye anakuja kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Beki Mamadou Doumbia ambaye wapo kwenye mazungumzo ya kuvunja mkataba wake baada ya kiwango chake kutowaridhisha mabosi wakubwa pamoja na benchi la ufundi la klabu hiyo.

Doumbia licha ya kuwa alikua anapata nafasi katika timu ya Taifa ya wachezaji wa ndani wa Mali ameshindwa kupata namba mbele ya mabeki Dickson Job,Bakari Mwamnyeto na Ibrahim Hamad ambao walikua chaguo la kocha Nasredine Nabi.

banner

Gift licha ya kuwa alikua ana uhakika wa namba katika kikosi cha Villa inampasa kupambana vya kutosha ili kupata nafasi katika kikosi cha Yanga sc ambacho kiko imara zaidi kulinganishwa na alikotoka.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited