Msafara wa kikosi cha Timu ya Yanga sc umefanikiwa kuwasili salama nchini Ethiopia kwa ajili ya mchezo wa kwanza wa raundi ya pili ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika dhidi ya Cbe SA utakaofanyika siku ya Jumamosi Septemba 14 mwaka huu.
Msafara huo ulianza safari mapema alfajiri ya leo ukiwa na baadhi ya mastaa wa kikosi cha kwanza huku wengine wataungana na kikosi moja kwa moja nchini humo wakitokea katika timu zao za Taifa zilizokua na michezo ya kujiandaa na michuano ya mataifa ya Afrika mwaka 2025 yatakayofanyika nchini Morocco.
Msafara huo wa Yanga sc utakutana na mastaa kama Stephane Aziz Ki,Duke Abuya,Prince Dube,Djigui Diarra sambamba na Cletous Chama na Kennedy Musonda ambao watatokea nchini mbalimbali kulingana na ratiba za michezo ya timu zao za Taifa.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Yanga sc inavaana na Cbe SA katika raundi ya pili baada ya kufanikiwa kuwafunga Vital O ya nchini Burundi kwa jumla ya mabao 10-0 katika michezo miwili ya raundi ya awali.