Home Makala Yanga sc,Wasudan Kumalizana Dar

Yanga sc,Wasudan Kumalizana Dar

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Zalan Fc kutoka Sudan Kusini imeomba kutumia uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam kama uwanja wa nyumbani katika mchezo wa hatua ya awali ya klabu bingwa Afrika dhidi ya Yanga sc.

Zalan Fc ambao ni mabingwa wa ligi kuu nchini kwao wamepangwa kucheza na Yanga sc katika mchezo wa kwanza ambao wao ndio wenyeji lakini wakaomba Caf mechi zote zifanyike jijini Dar es salaam kwa maana ya kwao hawana uwanja wenye hadhi ya kuchezewa michuano ya Caf.

Imethibitishwa kwamba ombi hilo limekubaliwa na Caf na sasa michezo yote miwili itapigwa jijini Dar es salaam huku ule wa awali Zalan Fc wakiwa wenyeji na ule wa marudiano Yanga sc watakua wenyeji wa mchezo huo.

banner

Zalan Fc ni timu changa huku ikiwa katika nchi ya Sudan Kusini ambapo hakuna miundombinu mizuri ya soka kiasi cha kushindwa kuwa mwenyeji wa michezo hiyo huku pia suala la bajeti nalo likiwa kikwazo kwao.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited