Kocha wa zamani wa yanga Mwinyi Zahera ametoa pongezi Yanga kwa usajili wa kiungo mpya kutoka Tp Mazembe Owen Bonyanga Ituku.
Zahera amesema kuwa anamfahamu vizuri sana mchezaji huyo hana mambo mengi anapokuwa uwanjani zaidi ya kuhitaji kupeleka mashambulizi mbele.
“Binafsi naamini safu ya ushambuliaji yanga ikiwa makini inaweza kushinda mabao mengi kwani Owen Bonyanga Ituku sio mchoyo hata kutoa pasi za mwisho hivyo nawatabiria makubwa”Alisema Mwinyi Zahera.
Alimalizia kwa Luc Eymael kocha mpya wa Yanga akiwashauli timu hiyo kumpa kocha huyo mahitaji yote kwani ni kocha mzuri aliyewahi kufundisha timu nyingi kubwa ikiwemo AS Vita kutoka Congo.