Home Masumbwi Kiduku kurudi Ulingoni

Kiduku kurudi Ulingoni

by Sports Leo
0 comments

Bondia Twaha kiduku anatarajiwa kurudi ulingoni mwezi ujao tarehe 26 kukipiga na bondia Alex Kabungu katika pambano la ubingwa ambalo litafanyika mkoano Morogoro.

Bondia huyo ambaye mara ya mwisho alipanda ulingoni Agosti mwaka jana akifanikiwa kumpiga Dulla Mbabe amekubali kucheza pambano hilo na Bondia huyo wa kimataifa kutoka Congo Drc.

“Ni kweli nimesaini kucheza pambano hilo ambalo litakuwa la mkanda wa ubingwa, naamini mkanda utabakia kwa sababu lazima nifanye maandalizi ya kutosha chini ya kocha wangu Pawa Ilanda.

banner

“Kila kitu tayari kimeshapangwa na promota juu ya siku ya pambano lakini maombi yangu ni kuweza kuwezasha pambano kufanyika mjini ili watu wengi waweze kuhudhuria taofauti na Magadu kwa sababu ni mbali na mjini,”Alisema Kiduka ambaye makazi yake ni mkoani Morogoro.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited