Home Soka Alliance,Malale Hamsini Washindwana

Alliance,Malale Hamsini Washindwana

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Alliance ya jijini Mwanza imeachana na kocha Malale Hamsini baada ya mkataba wa kocha huyo kufikia tamati na pande mbili kushindwa kuafikiana kuhusu mkataba mpya.

Awali Alliance walikua na mpango wa kumuongezea mkataba kocha huyo lakini baada ya pande mbili kukutana walishindwa kufikia muafaka hasa katika suala la maslahi hali iliyosababisha kocha huyo kuamua kuachana na timu hiyo iliyochini ya Meya wa jiji la Mwanza James Bwire.

Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo inaeleza kuwa ndani ya wiki hii benchi jipya la ufundi la klabu hiyo litatangazwa rasmi huku tarehe ya kuanza mazoezi na mahali rasmi pa kufanyia mazoezi haya vitatangazwa baadae huku zoezi la usajili likiendelea klabuni hapo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited