Home Soka Ansu Fati aibeba Barca dhidi ya Valencia

Ansu Fati aibeba Barca dhidi ya Valencia

by Dennis Msotwa
0 comments

Kinda wa Barcelona Ansu Fati ameiongoza klabu yake kuibuka na ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Valencia katika mchezo wa ligi kuu soka nchini Hispania(La liga) uliofanyika katika dimba la Camp Nou Jijini Barcelona.

Valencia walikuwa wa kwanza kujipatia bao dakika ya 5 kupitia kwa nahodha wake Jose Gaya,dakika ya 13 Fati aliisawazshia timu yake kwa shuti kali nje ya kumi na nane akimalizia pasi ya mguso kutoka kwa Memphis Depay.

Memphis Depay aliiongezea Barcelona goli la pili kwa mkwanju wa penati dakika ya 41 baada ya Asu Fati kufanyiwa madhambi ndani ya penati box na mlinzi Gaya.

banner

Philipe Coutinho aliyeingia kipindi cha pili aliihakikishia ushindi timu yake kwa kufunga goli la tatu dakika ya 85 na kumaliza ukame wa takribani miezi 11 bila kufunga goli la ligi.

Katika mchezo huo mcshambuliaji mpya wa timu hiyo Sergio Aguero alipata nafasi ya kuichezea timu hiyo kwa mara ya kwanza tangu ajiunge nayo kutoka Man City akiwa huru.

Barcelona wamepanda ya saba kwenye La liga wakiwa na pointi 15 pointi tano nyuma ya vinara Real Sociedad wenye alama 20 huku Barca wakiwa na faida ya mchezo mmoja mkononi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited