Kocha wa Simba sc Patrick Aussems alikua mkali na mwenye hasira baada ya kutoka katika kikao na viongozi wa klabu hiyo kilichofanyika katikati ya jiji la Dar es salaam zilizopo ofisi za mtendaji mkuu wa klabu hiyo Senzo Mazingisa.
Kocha huyo alionekana akifoka huku akiwa ameambatana na msaidizi wa tajiri wa klabu hiyo Barbra Hernandez huku akiwa mwenye hasira kali.
Kocha huyo aliitwa kujieleza baada ya kusimamishwa kwa siku kadhaa kufuatia kuonesha utovu wa nidhamu baada ya kuondoka nchini bila kutoa taarifa rasmi huku tetesi zikidai alikwenda kufanya mazungumzo na baadhi ya klabu ikiwemo Polokwane Fc ya afrika ya kusini.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.