Home Soka Azam Fc Yaizamisha Mtibwa Sugar

Azam Fc Yaizamisha Mtibwa Sugar

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imezidi kuzamisha jahazi la Mtibwa Sugar baada ya kuichapa mabao 2-0 ugenini katika uwanja wa Manungu Complex ulioko Turiani Morogoro katika mchezo wa ligi kuu ya soka ya Nbc uliofanyika Mei 06 2024.

Azam Fc ikianza na kikosi chake cha kila siku ilianza kupata bao dakika ya 20 baada ya krosi iliyopigwa na Ayoub Lyanga kupigwa kichwa na Dan Amoah ambaye alipiga kichwa kilichopanguliwa na kipa Mohamed Makaka na mpira kumkuta Feisal Salum ambaye aliutia nyavuni.

Licha ya Mtibwa kujitahidi kusawazisha bao hilo kipindi cha pili waliadhibiwa tena kwa shambulizi la kushtukiza ambapo mpira wa krosi ya chinichini ya Feisal Salum ulimkuta Gibril Silla ambaye alimchungulia kipa Makaka na kuandika bao la pili.

banner

Azam Fc sasa wamefikisha alama 57 nyuma ya Yanga sc iliyo kileleni na alama 65 baada ya timu zote kucheza michezo 25 ya ligi kuu huku Mtibwa Sugar ikiwa mkiani mwa msimamo na alama 17 katika michezo 25 ya ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited