Baada ya kugawana alama na Geita Gold Fc katika mchezo wa ligi kuu uliofanyika katika uwanja wa Nyakumbu mjini Geita klabu ya Azam Fc imewasili salama jijini Dar es salaam ikitokea mwanza tayari kuwakabili Yanga sc katika mchezo wa ligi kuu utakaofanyika katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es salaam.
Katika mchezo wa mwisho mkoani Geita sare ya 1-1 ilifanya Azam Fc kupoteza alama mbili huku Yanga sc wakiifunga Coastal Union mabao 3-0 mchezo wa mwisho uliofanyika jijini Dar es salaam.
Azam Fc inawalazimu washinde mchezo wa Jumapili ili wafikishe alama 40 na kupunguza pengo la uongozi kwa Yanga sc yenye alama 44 ikiwa na michezo 17 huku ikikumbukwa katika mchezo wa mwisho timu hizo zilitoka sare ya 2-2.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.