Home Soka Azam Fc Yarejea Dar Kuwakabili Yanga sc

Azam Fc Yarejea Dar Kuwakabili Yanga sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Baada ya kugawana alama na Geita Gold Fc katika mchezo wa ligi kuu uliofanyika katika uwanja wa Nyakumbu mjini Geita klabu ya Azam Fc imewasili salama jijini Dar es salaam ikitokea mwanza tayari kuwakabili Yanga sc katika mchezo wa ligi kuu utakaofanyika katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es salaam.

Katika mchezo wa mwisho mkoani Geita sare ya 1-1 ilifanya Azam Fc kupoteza alama mbili huku Yanga sc wakiifunga Coastal Union mabao 3-0 mchezo wa mwisho uliofanyika jijini Dar es salaam.

Azam Fc inawalazimu washinde mchezo wa Jumapili ili wafikishe alama 40 na kupunguza pengo la uongozi kwa Yanga sc yenye alama 44 ikiwa na michezo 17 huku ikikumbukwa katika mchezo wa mwisho timu hizo zilitoka sare ya 2-2.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited