Home Soka Barca vs Bayern hapatoshi UEFA

Barca vs Bayern hapatoshi UEFA

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Barcelona inatarajia kumenyana na mabingwa wa soka Ujerumani Bayern Munich katika mchezo wa kwanza wa kundi E katika michuano ya klabu bingwa barani Ulaya UEFA.

Miamba hiyo ya soka itacheza mchezo huo katika dimba la Nou Camp jijini Barcelona saa nne kamili usiku kwa saa za Afrika mashariki.

Mara ya mwisho timu hizo zilikutana hatua ya robo fainali mwaka 2020 ambapo Bayern waliibuka na ushindi wa mabao 8-2.hivyo mechi hiyo ni kama ya kisasi kwa Barca ambao kikosi chao hakitishii sana baada ya kuondoka kwa Lionel Messi na Antoine Giezmann.

banner

Jumla ya mechi 8 zinatarajiwa kupigwa hii leo,michezo mingine ni;

1.Young Boys vs Manchester United (saa 1:45 usiku)

2.Dynamo Kyiv vs Benfica (saa 4:00 usiku)

3.Villareal vs Atalanta (saa 4:00 usiku)

4.Chelsea vs Zenit St Petersburg (saa 4:00 usiku)

5.Malmo vs Juventus (saa 4:00 usiku)

6.Sevilla vs Salzburg (saa 1:45 usiku)

7.Lille vs Wolfsburg (saa 4:00 usiku).

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited