Klabu ya Simba imeanza mazungumzo na Beki wa Kati wa klabu ya Dynamos ya Zimbabwe na timu ya taifa ya Zimbabwe Patson Jaure mwenye umri wa miaka 30.
Simba wanamtaka beki huyo mwenye uzoefu ikiwa ni mlakati wa kuimarisha Kikosi chao hasa katika safu ya Ulinzi kwa ajili ya michuano ya Klabu bingwa Africa na ligi kuu Tanzania bara.
Kazi ya kumpata beki huyo inaweza isiwe ngumu kwa Simba SC Tanzania kwani wanaweza kumtumia kocha wao wa zamani Zdvradko Logarusic ambaye ndiye anayekinoa Kikosi cha timu ya Taifa ya Zimbabwe kitakachoshiriki fainali zijazo za CHAN,
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Kama hiyo haitoshi Simba bado wanaweza kumtumia Kiungo wao wa zamani Justice Majabvi kumshawishi beki huyo kujiunga na mabingwa hao wa Vodacom Premier league.