Home Soka Bruno Atua Man Utd

Bruno Atua Man Utd

by Sports Leo
0 comments

Hatimaye tetesi za muda mrefu kuhusu usajili wa kiungo Bruno Fernandes kutoka Sporting Lisbon kwenda Man United zimefika kikomo baada ya dili hilo kukamilika rasmi.

Sporting wamethibitisha taarifa za kumuuza kiungo wao Fernandes kwa kiasi cha £68m huku Man United wakilipa kiasi cha £46.6m kama malipo ya awali na zingine zitalipwa kama malipo ya nyongeza kutokana na vipengele mbalimbali.

Sporting watapata £4.2m endapo Man United watafanikiwa kupata nafasi ya kushiriki ligi ya mabingwa Ulaya msimu ujao.

Man United pia watalipa kiasi cha £12.6 endapo Fernandes atafanikiwa kuchukua tuzo binafsi na wakala wake pia atapokea £4.6m.

Sporting pia wameeleza kuwa wameweka kipengele cha kupata asilimia (10%) endapo Man United watamuuza Fernandes.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited