Timu mbalimbali zimeanza kuwasili Tanzania kuelekea kwenye mashindano ya Cecafa kwa Wanawake yatakayoanza Novemba 16-25,2019 Dar es Salaam.
Tayari timu za Burundi na Djibout zimetua jana Jumanne na kuelekea kwenye Hoteli zilizopangiwa.
Leo timu za Kenya na Ethiopia zinataraji kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Uganda wenyewe wanatarajia kuingia Kesho mchana sawa na Zanzibar huku pia tukiitarajia timu ya Sudan Kusini.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Wenyeji Tanzania Bara “Kilimanjaro Queens” mabingwa watetezi tayari wapo Kambini wakiendelea kujifua.