Kuna uwezekano mkubwa wa staa wa zamani wa Atletico Madrid na Chelsea Diego Costa kujiunga na timu ya Benfica Fc inayoshiriki ligi kuu nchini Ureno baada ya klabu hiyo kukubaliana na wakala George Mendez anayemsimamia mchezaji huyo.
Awali staa huyo aliyechagua kuichezea timu ya taifa ya Hispania badala ya Brazil alivunja mkataba na timu ya Atletico Madrid kwa makubaliano ya pande mbili huku akiwa na mawazo ya kurejea Brazil lakini uhusiano mzuri wa Mendez na Benfica umesababisha staa huyo kubadili mawazo.
Costa atalipwa kiasi cha paundi milioni 2.6 kwa mwaka katika mkataba wa miaka miwili atakaosaini katika klabu hiyo maarufu barani ulaya.