Home Soka Dante,Abdul Wapigwa “Stop” Yanga

Dante,Abdul Wapigwa “Stop” Yanga

by Sports Leo
0 comments

Inaelezwa kuwa mabeki wa timu ya Yanga sc Juma Abdul na Andrew Vicent “Dante” wamesimamishwa na uongozi wa klabu hiyo kwa muda usiojulikana baada ya kutoripoti kambini mjini Morogoro kwa muda mrefu.

Habari za ndani zinadai wachezaji hao wamegoma kushinikiza kulipwa madai yao ya fedha za usajili na mishahara wanazodai klabuni hapo baada ya kuongeza mikataba mwaka jana na mwaka juzi hali iliyowalazimu kugoma kuripoti kambini baada ya uongozi kutotimiza ahadi yao ya kuwalipa kabla ya msimu mpya kuanza huku wale wachezaji wa kigeni wakitimiziwa stahiki zao zote.

Mmoja ya wachezaji hao alidai wamegoma ili watimiziwe mahitaji hayo ndio wajiunge kambini kama wenzao,Mabeki hao hawajaripoti kambini sambamba na mkongwe Kelvin Yondani huku taarifa zikidai Yondani ana ruhusa maalumu kutoka kwa uongozi wa klabu hiyo ili kushughulikia.

banner

Taarifa zinadai uongozi wa klabu hiyo umeamua kuwasimamisha wachezaji kwa muda usiojulikana baada ya kuonesha utovu wa nidhamu kwa kutoripoti kambini na kuhusu madai yao uongozi ungeshughulikia huku wakiwa kambini na sio kuripoti katika vyombo vya habari.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited