Home Soka Feisal Kinara Ligi Kuu

Feisal Kinara Ligi Kuu

by Sports Leo
0 comments

Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Azam Fc Feisal Salum amekua kinara wa ufungaji wa mabao katika ligi kuu ya Nbc msimu mpaka sasa baada ya kufanikiwa kufunga mabao 11 katika michezo 19 aliyocheza na timu yake ya Azam Fc.

Katika mchezo wa Dodoma Jiji mchezaji huyo alifunga mabao mawili dakika za 63 na 64 na kufikisha idadi hiyo ya mabao akimpita kiungo mshambuliaji wa klabu ya Yanga sc Stephane Aziz Ki aliyefunga mabao 10 mpaka sasa licha ya kukosa zaidi ya michezo mitatu ya mwanzoni mwa ligi kuu iliyokua imesimama kutokana na kupisha michuano ya Afcon mwezi Januari.

Wengine walioko kwenye orodha ya ufungaji bora mpaka sasa ni Maxi Nzengeli wa Yanga sc mwenye mabao nane na aliyekua mshambuliaji wa Simba sc Jean Baleke ambaye ana mabao nane pia sambamba na Waziri Junior wa Kmc na Marouf Tchakei wa Ihefu Fc.

banner

Msimu uliopita Feisal akiwa Yanga sc alifanikiwa kufunga mabao sita na kutoa pasi tatu za magoli kwa nusu msimu aliocheza lakini sasa akiwa na klabu yake ya Azam Fc amejipata akifunga idadi hiyo ya mabao huku ikiwa bado msimu unaendelea.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited