Home Soka Feisal,Lamine Kuivaa Azam Fc

Feisal,Lamine Kuivaa Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Nyota wa nne wa timu ya Yanga wamerejea kikosini tayari kuongeza nguvu kuelekea mchezo wa Jumapili wa Ligi Kuu dhidi ya Azam FC.

Nahodha Lamine Moro, Feisal Salum na Dickson Job ambao walikuwa marejeruhi wamerejea kikosini na jana wamefanya mazoezi pamoja na wenzao.

Mlinda mlango Metacha Mnata aliyekuwa na matatizo ya kufiwa na mtoto wake nae amerejea kikosini.

banner

Msemaji wa klabu hiyo, Hassan Bumbuli amesema wanafahamu mchezo utakuwa mgumu kutokana na ubora wa Azam huku wakijinasibu kuondoka na alama zote tatu.

“Tunahitaji kushinda mechi zetu zote za Ligi zilizobaki, tunajua mchezo utakuwa mgumu lakini tupo tayari kwa mchezo na tuna uhakika wa kubaki na alama zote tatu,” amesema Bumbuli.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited