Home Soka Fifa Yamtambua Sasi

Fifa Yamtambua Sasi

by Sports Leo
0 comments

Hery Sasii ni miongoni mwa waamuzi 17 walioteuliwa kuvaa beji za Shirikisho la Soka la kimataifa (FIFA) mwakani.

Taarifa ya waamuzi hao imetolewa na Shirikisho la Soka nchini (TFF) na kuwataja wengine kwa waamuzi wa kati kuwa ni Florentina Zablon, Jonesia Rukyaa, Martin Saanya, Mfaume Nassoro na Ramadhan Kayoko.

Waamuzi wasaidizi ni Abdulaziz Ally, Ferdinand Chacha, Frank Komba, Hellen Mduma, Janet Balama, Kassim Mpanga, Mbaraka Haule, Mohamed Mkono na Soud Lila.

banner

Siku za karibuni mwamuzi Henry Sasi amekua na maamuzi tata katika michezo aliyochezesha kiasi cha kuwatia hofu mashabiki kuhusu kiwango cha mwamuzi huyo hasa baada ya kuipa Simba sc penati ambayo haikua sahihi katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Kmc.

Credit:Dominick Salamba

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited