Home Soka Gomez Kupasuliwa Leo

Gomez Kupasuliwa Leo

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Everton ya nchini England, imethibitisha kuwa mchezaji wao Andre Gomes atafanyiwa upasuaji leo hii nchini humo.

Gomes alivunjika mguu wake wa kulia siku ya jana katika mchezo wa ligi dhidi ya timu ya Tottenham Hotspurs.

Katika mchezo huo, Heung Son wa Spurs alioneshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja, baada ya kumchezea rafu Gomes iliyompelekea kwenda kugongana na beki wa Spurs, Serge Aurier na kusababisha kuvunja mguu wake.

Mreno huyo alitolewa kwa msaada wa machela katika uwanja wa Godson Park, kabla ya kupelekwa katika hospital ya Aintree kwa matibabu na vipimo zaidi.

Klabu yake ya zamani Barcelona imemtumia salamu za pole pamoja na mastaa mbalimbali duniani akiwemo Lucas Digne beki wa Barcelona ambaye walicheza wote Nou camp.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited