Home Soka Griezman Arejea Atletico Madrid

Griezman Arejea Atletico Madrid

by Sports Leo
0 comments

Mabingwa wa La Liga, Atletico Madrid wamefanikiwa kumsajili tena mshambuliaji, Antoine Griezmann kutoka Barcelona kwa mkopo Miaka miwili iliyopita mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alihama klabu hiyo baada ya Barca kulipa kifungu chake cha uhamisho wa pauni milioni 107.

Lakini wakati wa mchezaji huyo wa miaka 30 huko Nou Camp umekuwa wa kukatisha tamaa kwani alifunga mabao 35 katika michezo 102 na akashinda Ubingwa wa Copa del Rey pekee…. Amekuwa mchezaji wa 11 kuondoka Barcelona yenye shida ya kifedha msimu huu, pamoja na Lionel Messi aliyejiunga na Paris St-Germain.

Griezmann atakuwa mchezaji wa tatu kuuzwa siku ya mwisho ya uhamisho kutoka Barcelona. Mlinzi wa kulia Emerson Royal alijiunga na Tottenham kwa pauni milioni 25.8 na kiungo wa kati kijana Ilaix Moriba alihamia RB Leipzig kwa pauni milioni 13.7…Msimu uliopita Atletico ilimsajili mshambuliaji Luis Suarez kutoka Barcelona na aliisaidia timu ya Diego Simeone kushinda La Liga.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited