Home Soka GSM waidhamini ligi kuu

GSM waidhamini ligi kuu

by Sports Leo
0 comments

Kampuni ya GSM wameingia mkataba wa miaka miaka miwili na shirikisho la soka nchini kupitia bodi ya ligi kudhamini ligi kuu soka Tanzania Bara wenye thamani ya Tsh bilioni 2.1.

Hafla ya utiaji saini mkataba imefanyika hii leo katika hoteli ya kitalii ya Serena jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi wa uwekezaji wa GSM Injia Hersi Said ndiye aliyeiwakilisha kampuni hiyo katika tukio hilo huku kwa upande wa TFF lilisimamiwa na makamu wa rais Athumani Nyamlani.

banner

                                           

Hatua hiyo ni katika harakati za bodi ya ligi kuongeza thamani ya ligi kuu kwa kuhakikisha ongezeko la wawekezaji ambao kwa nafasi zao watatatua changamoto mbalimbali zinazoikabili ligi hiyo.

GSM inaungana na kampuni ya Azam,Shirika la habari nchini TBC pamoja na benki ya NBC kama wadhamini rasmi wa ligi kuu inayoendelea.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited