Home Soka Gsm Yamrejesha Lamine

Gsm Yamrejesha Lamine

by Sports Leo
0 comments

Kampuni ya Gsm imefanikiwa kumrejesha beki wa klabu ya Yanga sc Lamine Moro baada ya kusaidia mazungumzo ya kumaliza matatizo baina ya mchezaji huyo na klabu hiyo.

Lamine aliondoka Jangwani baada ya kuandika barua ya kuvunja mkataba kufuatia kucheleweshewa baadhi ya stahiki zake ikiwemo mishahara na posho hivyo kuamua kuvunja mkataba na klabu hiyo.

Hata hivyo licha ya kuonyesha nia ya kuvunja mkataba huo klabu hiyo ilijitahidi kumrejesha mchezaji huyo hasa baada ya kupata tetesi za kukaribia kujiunga na Simba mpaka walipofanikiwa baada ya kampuni ya Gsm kuingilia kati kumaliza tatizo hilo.

banner

Lamine tayari amerejea nchini na tayari amemalizana na uongozi wa klabu hiyo huku akithibitisha kuendelea kutumikia mkataba wake na klabu hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited