Home Soka Hazard kurejea Chelsea?

Hazard kurejea Chelsea?

by Dennis Msotwa
0 comments

Nahodha wa timu ya Taifa ya Ubelgiji Eden Hazard huenda akapata nafasi nyingine ya kurudisha kiwango chake kilichozoeleka baada ya klabu yake ya zamani Chelsea kufikiria kumrudisha tena darajani.

Mchezaji huyo amekuwa kwenye kiwango duni tangu ajiunge na Real Madrid misimu miwili iliyopita na kwa muda mrefu amekuwa kwenye meza ya matibabu kutokana na majeraha ya mara kwa mara.

Chelsea wanaandaa mpango wa kumsajili upya Hazard ili akakiongezee nguvu kikosi hicho kilichokosa makali katika safu ya ushambuliaji kutokana na wachezaji wa eneo hilo kuwa na viwango vya kupanda na kushuka.

banner

Real Madrid ina mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Paris St German Kylian Mbappe kama mbadala wa Eden Hazard katika dirisha lijalo la usajili.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited