Mshambuliaji wa Nigeria Odian Ighalo amethibitisha kuachana na klabu ya Manchester United aliyoichezea kwa kipindi cha muda wa mwaka mmoja kwa mkopo kutoka klabu ya Shanghai Shenhua ya nchini China.
Ighalo 31 ameichezea Man Utd mechi 23 akifunga mabao 5 anaelekea kujiunga na klabu ya Al-Shabab ya nchini Saud Arabia ambako imebaki taratibu za kiafya kukamilisha usajili huo.
Ighalo alitakiwa kurudi nchini China lakini klabu yake inayommiliki ya Shangai Shengua ilimruhusu kuzunguma na klabu ya Al shabab ili kukamilisha usajili huo.