Klabu ya Manchester United imefikia makubaliano na klabu ya Shangai Shenghua juu ya mchezaji Odian Ighalo ambaye atasalia klabuni hapo hadi julai 31 mwisho wa msimu wa ligi kuu nchini Uingereza.
Awali Staa huyo Raia wa Nigeria alisaini mkataba wa mkopo wa muda wa miezi sita uliokua unaisha Mei 31 lakini kusimamishwa kwa ligi kuu ya Uingereza kutokana na kusambaa kwa ugonjwa wa homa ya Mapafu unaosababishwa na Virusi vya Corona ambapo sasa itabidi ligi hiyo kumalizika julai.
Ighalo ameonekana kufurahia maisha klabuni hapo huku pia akifunga magoli manne katika mechi nane hali inayowafanya United kufikiria kumsajili jumla japo tayari klabu yake imemwekea mshahara wa Paundi laki 4 kwa wiki ili aongeze mkataba wa kubaki nchini China.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.