Home Soka Ighalo Kumalizia Msimu United

Ighalo Kumalizia Msimu United

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Manchester United imefikia makubaliano na klabu ya Shangai Shenghua juu ya mchezaji Odian Ighalo ambaye atasalia klabuni hapo hadi julai 31 mwisho wa msimu wa ligi kuu nchini Uingereza.

Awali Staa huyo Raia wa Nigeria alisaini mkataba wa mkopo wa muda wa miezi sita uliokua unaisha Mei 31 lakini kusimamishwa kwa ligi kuu ya Uingereza kutokana na kusambaa kwa ugonjwa wa homa ya Mapafu unaosababishwa na Virusi vya Corona ambapo sasa itabidi ligi hiyo kumalizika julai.

Ighalo ameonekana kufurahia maisha klabuni hapo huku pia akifunga magoli manne katika mechi nane hali inayowafanya United kufikiria kumsajili jumla japo tayari klabu yake imemwekea mshahara wa Paundi laki 4 kwa wiki ili aongeze mkataba wa kubaki nchini China.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited