Home Soka Kaseja Aibukia Twiga Stars

Kaseja Aibukia Twiga Stars

by Sports Leo
0 comments

Kipa wa timu ya taifa ya Tanzania(Taifa stars) Juma Kaseja ameibukia kwenye mazoezi ya timu ya taifa ya wanawake Tanzania (Twiga stars) akiwanoa makipa wa timu hiyo.

Kipa huyo mkongwe aliyetoka kuisaidia Taifa stars kushinda mchezo dhidi ya Sudan na kufanikiwa kukata tiketi ya fainali za michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani ameshiriki mazoezi ya timu hiyo inayojiandaa na michuano ya chalenji ambayo itafanyika nchini kuanzia novemba 14-23 desemba.

“Mimi ni Mtanzania, na nina jukumu la kuisaidia Tanzania, nimemaliza majukumu ya Stars, jana (juzi) nimecheza mechi (JKT Tanzania vs KMC), na leo nimeamua kuja kufanya mazoezi na dada zetu, mara nyingi nimekuwa nikiwasaidia, ili waweze kutimiza ndoto zao,” alisema Kaseja.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited