Timu ya taifa ya Wanawake ya Tanzania Bara(Kilimanjaro queens) imeibuka na ushindi wa magoli 4-0 dhidi ya Burundi katika mchezo wa michuano ya kombe la chalenji kwa wanawake inayoendelea nchini.
Hii ni mechi ya pili kwa Kilimanjaro queens kuibuka na ushindi baada ya hapo awali kuwafunga Sudan Kusini jumla ya mabao 9-0 mchezo uliofanyika uwanjani hapo chamazi.
Mabao ya Kilimajaro katika mchezo wa leo yalifungwa Donisia Minja dakika za 35′ na 75′ huku Asha Rashid pia akifunga dakika ya 72 na Mwanahamis Omary dakika ya 86 na kufanya timu hiyo kuwa na magoli 13 ya kufunga katika michezo miwili.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.