Timu ya Taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) imekubali kipigo cha bao moja kutoka kwa Harambee Stars katika mchezo wa michuano ya chalenji uliofanyika katika uwanja wa KCCA nchini Uganda.
Kenya walifanikiwa kupata bao pekee la mchezo huo dakika ya nne ya mchezo likifungwa na Hassan Abdalah baada ya mabeki wa Stars kuzembea.
Bao hilo lilidumu mpaka mwisho wa mchezo licha ya Stars kujitahidi kutafuta goli la kusawazisha lakini uimara wa mabeki wa kenya ulikua mwiba kwa washambuliaji wa Stars wakiongozwa na Paul Nonga.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.