Home Soka Kiungo Mtibwa,Azam Afariki Dunia

Kiungo Mtibwa,Azam Afariki Dunia

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa zamani wa Azam fc na Mtibwa sugar Ibrahim Rajabu Jeba amefariki dunia akiwa visiwani  Zanzibar alikokua akiichezea timu ya Chuoni fc ya visiwani humo.

Jeba aliyewahi kuichezea Azam fc,Mtibwa sugar na timu ya taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) amefariki akiwa visiwani humo baada ya kuugua na kulazwa katika hospitali ya Mnazi mmoja iliyopo visiwani humo.

Kiungo huyo enzi za uhai wake alisifika kwa soka la uhakika akitumia akili na nguvu kiasi cha kuwa tishio kwa viungo wengi nchini waliokua wakikutana nae uwanjani.

banner

Timu ya chuoni fc anayoichezea kiungo huyo imethibitisha kifo cha mchezaji huyo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited