Home Soka Kocha Yanga Afunga Ndoa

Kocha Yanga Afunga Ndoa

by Sports Leo
0 comments

Kocha mkuu wa timu ya Yanga, Luc Eymael leo amefunga ndoa ya kimya kimya na mpenzi wake Patricia Abbruzzese nchini Afrika Kusini kutokana na mlipuko wa homa ya virusi vya Corona.

Eymael amesema ndoa hiyo ilifungwa katika kanisa la Harre nchini humo lakini ilikuwa binafsi kwakua hakuruhusiwi mikusanyiko yoyote.

Kocha huyo ameiambia Wapendasoka kuwa baada ya kupata nafasi katika kipindi ligi imesimama akaona amalize kabisa suala la ndoa.

banner

“Ni kweli nimefunga ndoa lakini ilikuwa ni binafsi kwakua kuna mlipuko wa virusi vya Corona, tulienda kanisani tu tumemaliza tunashuru,” alisema Eymael.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited