Home Soka Kotei Huru Kuja Bongo

Kotei Huru Kuja Bongo

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya ligi kuu nchini Belarus, FC Slavia Mozyr wameachana na kiungo wa kimataifa wa Ghana, James Agyekum Kotei baada ya miezi mitano tu Kotei anaondoka kwenye Klabu hiyo kwa makubaliano ya pande zote kwani alishindwa kupata nafasi ya kuanza XI tangu ajiunge mnamo Januari 2020.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alijiunga na Mazyr baada ya kuachana na miamba wa soka Afrika Kusini, Kaizer Chiefs FC kwa kukosa muda wa kucheza Nyota wa zamani wa Liberty Professional ameshindwa kuanza hata game moja kwenye Ligi Kuu ya Belarus msimu huu baada ya mechi 13 Alikuwa kwenye benchi mara tatu tu.

Kotei aliwahi kuitumikia Simba SC ya nyumbani Tanzania kabla ya kuelekea Afrika Kusini baada ya kucheza kwa mafanikio Akiwa na Mnyama, alitwaa ubingwa wa Tanzania mara mbili mfululizo na pia alifika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa ya CAF msimu wa 2018/2019.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited