Inaelezwa kuwa kocha wa zamani wa Yanga sc Mzambia George Lwandamina ndio kikwazo cha mchezaji Geoffrey Mwashiuya kutosaini timu yeyote hapa nchini akilisikilizia simu ya kocha huyo ambaye anataka akajiunge na Timu anayoifundisha ya Zesco ya Zambia.
Lwandamina anayesifika kwa kutumia wachezaji vijana na kutandaza soka safi aliondoka Yanga na kwenda kujiunga na waajiri wake wa zamani wa Zambia hivyo anamfahamu winga huyo kinagaubaga baada ya kumfundisha jangwani.
Mwashiuya mwenye uwezo wa kucheza winga na mshambuliaji namba mbili(namba 10) anawindwa na baadhi ya timu za ndani kama vile Alliance fc,Jkt Tanzania ambazo hazina budi kumsubiria mpaka mchezaji huyo atakapopata maelekezo kutoka kwa Lwandamina ya ama akajiunge na Zesco au asaini timu nyingine.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.