Home Soka Makambo arejea Yanga

Makambo arejea Yanga

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Heritier Makambo amejiunga tena Yanga sc kwa mkataba wa miaka miwili akiwa mchezaji huru akitokea klabu ya Horoya ya Guinea.

Mpachika mabao huyo aliyewahi kuwika Jangwani na kuwa kipenzi cha mashabiki wa timu hiyo alitimkia nchini Guinea mwaka 2019 kujiunga na Horoya baada ya kuifungia Yanga mabao 17.

Makambo anatajwa kuchukua nafasi ya Mghana Michael Sarpong anayehusishwa kutemwa na mabingwa hao wa kihistoria wa Tanzania baada ya jezi yake namba 19 kupewa Makambo.

banner

Yanga kwa kwasasa imeshasajili mastraika wawili Makambo na Mayele. kuboresha safu ya ushambuliaji iliyoonekana kusuasua msimu uliopita.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited