Home Soka Man Utd Inajipigia Tu

Man Utd Inajipigia Tu

by Sports Leo
0 comments

Manchester United imeibuka kinara  wa kundi L baada ya hapo jana usiku kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Az Alkamaar katika mchezo wa ligi ya ulaya uliofanyika katika uwanja wa Old Trafford jijini Manchester.

United ililazimika kwenda mapumziko bila bao baada ya wageni kujitahidi kutoa upinzani wa  kutosha lakini kipindi cha pili united ilipata mabao kupitia kwa Ashley Young dakika ya 52 na Mason Greenwood 58′ 64′ huku Juan Mata akipachika bao la nne kwa njia ya penati.

Kwa ushindi huo united imeibuka kinara wa kundi hilo baada ya kuwa na pointi 13 katika michezo sita huku Az Alkmaar akiwa nafasi ya pili.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited