Home Soka Man Utd Yaizunguka Real Madrid

Man Utd Yaizunguka Real Madrid

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Man utd imeanzisha mazungumzo na Ajax juu ya kumsajili kiungo Donny Van De Beek kutokana na taarifa nchini Uholanzi.

Awali iliripotiwa kwamba Real Madrid imekubaliana na Ajax kiasi cha paundi milioni 44 kumsajili kiungo huyo na ilibaki kukamilisha vipimo vya afya tu lakini dili hilo mpaka sasa limesimama kufuatia matatizo ya kifedha yaliyosababishwa na Virusi vya Corona.

Man utd inataka kutumia mwanya huo kukamilisha dili hilo huku uhusiano wake mzuru na mtendaji mkuu wa Ajax Edwin Van De Sar ukichagiza dili hilo kukamilika mapema huku United ikitaraji kukamilisha dili hilo kwa bei ya chini kuliko Real Madrid.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited