Klabu ya Man utd imeanzisha mazungumzo na Ajax juu ya kumsajili kiungo Donny Van De Beek kutokana na taarifa nchini Uholanzi.
Awali iliripotiwa kwamba Real Madrid imekubaliana na Ajax kiasi cha paundi milioni 44 kumsajili kiungo huyo na ilibaki kukamilisha vipimo vya afya tu lakini dili hilo mpaka sasa limesimama kufuatia matatizo ya kifedha yaliyosababishwa na Virusi vya Corona.
Man utd inataka kutumia mwanya huo kukamilisha dili hilo huku uhusiano wake mzuru na mtendaji mkuu wa Ajax Edwin Van De Sar ukichagiza dili hilo kukamilika mapema huku United ikitaraji kukamilisha dili hilo kwa bei ya chini kuliko Real Madrid.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.