Home Soka Manara Akabidhiwa Hamasa

Manara Akabidhiwa Hamasa

by Sports Leo
0 comments

Bosi mpya wa klabu ya Simba sc Senzo Masingizi ameoneshwa kufurahishwa na kazi ya Afisa habari wa klabu hiyo Haji Manara kuhamasisha mashabiki wa timu hiyo kujaa uwanjani na kuipenda timu yao.

Bosi huyo raia wa Afrika Kusini ambaye ametambulishwa leo mbele ya waandishi wa habari ameonesha kumkubali manara baada ya kumkabidhi kazi ya kuhamasisha mashabiki wa timu hiyo.

“Nimekua nikimfatilia Haji manara,mambo anayofanya kwenye vyombo vya habari ndivyo inavyotakiwa,wahamasishe mashabiki wa simba wajae uwanjani na waipende timu yao”.

banner

Kauli hiyo ya bosi mpya imeonesha kujibu maswali ya wadau wengi wa michezo kuhusu hatma ya Manara klabuni hapo baada ya hivi karibuni klabu hiyo kutangaza nafasi za kazi ikiwemo ya Afisa habari ambayo ilikua ikishikiliwa na manara.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited