Home Soka Mbombo Atua Nkana Fc

Mbombo Atua Nkana Fc

by Sports Leo
0 comments

Aliyekuwa mshambuliaji wa Azam FC, Idriss Mbombo amejiunga na klabu ya Nkana FC ya Zambia na kutambulishwa rasmi kuwa mchezaji wa klabu hiyo kwa mkataba ambao haukuwekwa wazi na kutambulishwa siku ya ijumaa na Mtendaji mkuu wa klabu hiyo Kelvin Mutafu.

Mshambuliaji huyo aliomba kuvunja mkataba wake ambao ulisalia na klabu ya Azam FC ili awe mchezaji huru ambapo muda mchache alisafiri haraka kwenda nchini Zambia kujiunga na Nkana ambapo alijumuika na mastaa wengine watatu katika utambulisho huo.

banner

Mshambuliaji huyo ameondoka Azam Fc baada ya kukosa nafasi katika kikosi cha kwanza ambapo kocha Yousouph Dabo anapenda zaidi kumtumia Prince Dube kama mshambuliaji wake wa kati huku akisaidiwa na Allasane Diara na mara nyingi Mbombo hukaa jukwaani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited