Home Soka Metacha Njia Nyeupe Yanga sc

Metacha Njia Nyeupe Yanga sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Muda wowote kuanzia sasa, kipa Metacha Mnata anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kukipiga Yanga.

Kipa huyo hivi karibuni aliingia kwenye mgogoro na timu hiyo mara baada ya kuandika ujumbe wa kuaga saa chache baada ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Polisi Tanzania uliomalizika kwa Yanga kutoka sare ya bao 1-1.

Inasemekana kipa huyo ndani ya wiki hii kuanzia leo Jumanne, huenda akapewa mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kukipiga Yanga, huku pia akirudishwa kikosi cha kwanza baada ya Farouk Shikalo kuonekana kuwa na makosa ya wazi.

banner

Cc:Sportsextra

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited