Home Soka Milioni 50 Zamshusha Ambundo Yanga sc

Milioni 50 Zamshusha Ambundo Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Dodoma jiji Fc Dickson Ambundo amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na klabu ya Yanga sc mara baada ya mkataba wake na klabu hiyo kufika mwisho mwezi juni mwaka huu.

Ambundo alikua anawindwa na klabu kubwa zote nchini lakini Yanga sc wamefanikiwa kumsajili kupitia kwa meneja wa mchezaji huyo aliyelainisha dili hilo huku kiasi hicho cha fedha kikimaliza mjadala ambapo kiungo huyo alikubali kusaini huku akisubiri kutambulishwa tu.

Yanga sc imepata urahisi wa kukamilisha dili hilo huku uwepo wa viongozi wakuu wa klabu hiyo jijini Dodoma katika semina ya mabadiliko kwa wabunge ukirahisisha dili hilo kukamilika pamoja na uhusiano mzuri baina ya mbunge wa Dodoma Anthony Mavunde.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited