Home Soka Mkude Aondolewa Stars

Mkude Aondolewa Stars

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha Mkuu wa Taifa Stars Ettiene Ndairagije amempa ruhusa Kiungo Jonas Mkude kuondoka kwenye Kambi ya Kikosi hicho kwenda kushughulikia masuala yake ya kifamilia.

Mkude alitoa taarifa kwa Kocha Ndairagije kuomba ruhusa ya kutojiunga Kambini ili kushughulikia masuala ya kifamilia,ruhusa ambayo alipewa kabla ya kuanza kwa Kambi Jumamosi.

Jana Jumatatu Mkude aliripoti Kambini na kumueleza Kocha Ndairagije kuwa bado hajamaliza masuala anayoshughulikia hivyo Kocha amempa ruhusa nyingine ya kumaliza jambo hilo linalomkabili.

banner

Kulingana na muda mfupi uliobaki kuelekea mchezo dhidi ya Equatorial Guinea Kocha Ndairagije hataweza kuongeza mchezaji mwingine.

Taifa Stars inacheza Ijumaa saa 1 usiku Uwanja wa Taifa mchezo wa kwanza hatua ya makundi kufuzu Afcon 2021.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited