Home Soka Molinga Aikoa Yanga

Molinga Aikoa Yanga

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji wa Yanga David Molinga ameiokoa timu hiyo na kipigo baada ya kufunga mabao mawili ya kusawazisha kufuatia kufunga mabao 3-1 mpaka dakika ya 58 ya mchezo dhidi ya Polisi Tanzania uliofanyika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Yanga walianza kupachika bao la uongozi dakika ya 6 kupitia kwa Mrisho Ngasa aliyemalizia krosi ya Juma Abdul bao lililodumu mpaka dakika ya 35 ambapo Ditram Nchimbi alisawazisha bao hilo na kufunga mengine mawili dakika za 55’na 58′.

Molinga alisaawazisha mabao hayo dakika ya 65 baada ya kumalizia mpira ulioshindwa kuokolewa na kipa wa Polisi na kisha dakika ya 69 alifunga tena kwa kiki ya faulo.

banner

Yanga leo ilimkosa kocha Mwinyi Zahera ambaye ameanza kutumikia adhabu ya kukosa mechi tatu baada ya kutovaa nadhifu katika mechi dhidi ya Ruvu shooting ambayo yanga ilipoteza pamoja na kutoa lugha isiyo na staha kwa shirikisho na soka nchini pamoja na bodi ya ligi kuu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited