Home Soka Moroko Aikacha Mbao

Moroko Aikacha Mbao

by Dennis Msotwa
0 comments

Uongozi wa Klabu ya Mbao FC umekubaliana na kocha wao mkuu Hemed Suleiman Morocco kuvunja mkataba wa kuendelea kuifundisha klabu hiyo yenye makao yake makuu mkoani Mwanza.
Inasemekana chanzo cha kuvunja mkataba huo ni mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha ya timu hiyo ambayo
kwa sasa inashika nafasi ya 18 kwenye msimamo ikiwa na alama 19 baada ya michezo 22 ya ligi kuu Tanzania bara.
Tangu Jana Kocha Morocco alithibitisha kwamba yeye na msaidizi wake Abdulmutik wameondoka jijini mwanza na sasa wako kwao Visiwani Zanzibar huku akisema pande zote mbili zimeachana kwa Amani baada ya kukubaliana kuvunja mkataba.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited